/home/mhubiriw/public_html/bwana.php on line 24
" style="color:
Warning: Undefined array key "font" in /home/mhubiriw/public_html/bwana.php on line 25
">

Habari njema

Tubuni

Ufalme wa yesu

Yesu na ufufuo

Yesu ndiye kristo

Mche mungu

Ubatizo wa maji mengi

Yesu ni bwana

Watumishi Yesu

 


"Kwa sababu, ukimkiri yesu kwa kinywa chako ni bwana na kuamini moyono mwako mungu alimfufua ktk wafu utaokokoka." . Warumi: 10: 8- 9

Sikilizeni enyi wafanyazi wa kimataifa mkimkiri yesu kwa vinywa vyenu ya kuwa ni bwana na mkiamini mioyoni mwenu mungu alimfufua yesu ktk wafu mtaokokoka. Yesu atawaokoa kutokaka maisha ya dhambi mnayoishi ya anasa kama pombe , rushwa , dhuluma ufisadi, uongo n.k atawapa asili yake mkipokea maisha yake yesu hakika mtavaa haki yake yeye hakuwahi kufanya dhambi hakuwahi kupokea rushwa wala kunaswa na mwanamke mwenye mitego.

Kumkiri yesu kwa kinywa chako ni bwana maana yake ni kukubali kwa moyo wewe ni mtumishi wake na hutaitumikia dhambi sikuzote za maisha yako kuanzia leo kama utamkiri ni bwana yaani utaachana na bwana dhambi akuitaye kila jioni baa na mwisho wa juma disko.Kuamini mungu alimfufua yesu ktk wafu ni kukubali kwa moyo mungu anao huo uwezo wa kumfufua hata mtu aliyekufa wengi hawajawahi shuhudia inawezekana nawe ni mmojawapo yapasa kuamini, kama alimfufua yesu na unaamini basi huyo mungu atakufufua na wewe kama utakubali kumtumikia na kumfuata yesu siku zote za maisha yako na huko ndiko kuokoka na maisha ya dhambi.

Yesu alikufa kwa ajili ya wenye dhambi watumishi wa mungu kama wewe mwenye kiu ya kumtumikia mungu ila huujui uweza wake ili akupatanishe na baba yake ambaye ndiye mungu aliyekuumba wewe mfanyakazi wa kimataifa. Hivyo anakuita upatane naye kwa kuamini yeye alikupenda sana wewe hata akamtoa mwanawe yesu afe ili wewe upate kuokolewa kutoka ktk dhambi au maisha ya dhambi akupe maisha ya haki ya mwanaye yesu aliyeishi bila kutenda dhambi kwa kufanya mapenzi ya mungu yaani baba yake.

Ikiwa unaamini yesu alisulubiwa na kufa kwa ajili ya wenye dhambi wa kimataifa kama wewe wapate kuokoka na maisha ya dhambi maisha ya kunuka rushwa , ufisadi, matukano, wanawake wenye mitego, anasa za dunia na umeamua leo kumgeukia yesu na kumfuata kwa kuachana na maisha ya dhambi na u tayari kupokea maisha ya uzima na haki ya yesu yaliyo huru mbali na dhambi na kuachana na ya kwako ya dhambi bofya Kuokoka

<||---kurudi nyuma <<<||>>> kuendelea mbele---||>

                                                       Mark: 16: 14 - 18