Tafakari
Mhubiri wa Kimataifa
Mahubiri
Kuokoka
Ushauri
Maombi
Shuhuda
Maarifa
Kusudi la Injili ya Kimataifa
Changia Injili ya Kimataifa
Matangazo/Shukrani
Burudani za Injili
|
Kusudi la mahubiri ya injili ya kimatataifa ni kwa watu wa kimataifa ktk dunia waliomo ktk nchi zote zilizomo ktk kila bara kumbuka mabara yapo saba
Ni wenye dhambi hasa wafanyakazi wafanyao kazi kimataifa wengi waokolewe yaani waokoke kwa kumwanini Yesu aliyesulubiliwa kwa ajili ya dhambi zao na baada ya siku tatu alifufuka awape haki ya maisha yake kwa toba, ubatizo wa maji mengi na ujazo wa roho
mtakatifu kwa jina lake. (matendo ya mitume 2:38 na marko 16:16).
"Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha roho mtakatifu"
Yesu anawatafuta apate kuwabadilisha kutoka ktk maisha ya dhambi hata ya haki mfano; kutoka maisha ya rushwa hadi kuacha rushwa, anasa(disko,ulevi) hadi kuacha maisha ya anasa, maisha ya kuzivunja amri kumi za mungu kama usizini hadi kuzishika yaani kutozini.
Neema na mahubiri ya injili ya kimataifa na ishara za kuyathibitisha: Alizopewa mhubiri wa kimataifa lameck lister na Yesu ni kuwahubiri habari njema za yesu wafanyakazi wa kimataifa wakiwepo watangazaji wa habari za kimataifa na waandishi,wanamichezo wa kimataifa kama tenesi, mpira, basketball; waalimu ktk shule za kimataifa na mahakama za kimataifa; wafanyakazi wa kimataifa ktk mashirika ya kimataifa kama yale ya Ndege za usafiri,madreva na watunza maazingira na maktabta ktk mashule ya kimataifa, mahakimu na watenda kazi ktk mahakama za kimataifa,maprofessa na watenda kazi ktk vyuo vya kimataifa, wapelelezi wa kimataifa duniani na wale wafanyabiashara wa kimataifa kama wale wa madini n.k. Yesu awaita muokoke na anawapenda sana.
Namshukuru mungu:
Baba wa bwana Yesu kwa wale watakaosoma tovutu hii na kujaliwa neema kuwa wa Yesu mwanaye. Asante Yesu wangu kwa wale wote watakaookoka ktk dhambi na kudumu sikuzote kutembea ktk imani ya yesu kristo kama mfalme, bwana na mwokozi wa maisha yao kwa kumnyenyekea sikuzote za maisha yao pamoja kwa kumfuata na kumtii msaidizi roho mtakatifu. |